• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 7:55 AM
Tottenham wajinasia kipa matata Guglielmo Vicario

Tottenham wajinasia kipa matata Guglielmo Vicario

Na MASHIRIKA

TOTTENHAM Hotspur wamemsajili kipa matata raia wa Italia, Guglielmo Vicario, kwa miaka mitano kutoka kikosi cha Empoli kinachoshiriki Ligi Kuu ya Italia (Serie A).

Anakuwa mchezaji wa pili baada ya kiungo raia wa Uswidi, Dejan Kulusevski, kutua kambini mwa Spurs chini ya kocha mpya Ange Postecoglou.

Vicario, 26, aliridhisha sana katika kipindi cha miaka miwili ya kuhudumu kwake kambini mwa Empoli na aliitwa kambini mwa Italia kwa michuano ya kimataifa kwa mara ya kwanza mnamo 2022-23.

Nahodha wa Spurs na kipa nambari moja kambini mwa kikosi hicho, Hugo Lloris, amesalia na miezi 12 pekee katika mkataba wake wa sasa na Spurs wanaoamini kuwa Vicario anaweza kucheza boli kuanzia safu ya ulinzi.

Vicario alianza kusakata soka kitaaluma akivalia glavu za Udinese na aliwahi pia kuhudumu kambini mwa Cagliari, Perugia na Venenzia kabla ya kutua Empoli mnamo Julai 2021 baada ya kikosi hicho kupandishwa daraja kushiriki Ligi Kuu ya Italia.

Empoli walitarajiwa kupigania fursa ya kusalia ligini wakiwa miongoni mwa vikosi vya mwisho kwenye jedwali la Seria A. Hata hivyo, Vicario aliwasaidia pakubwa na wakaambulia nafasi ya 14 mnamo 2022-23, hiyo ikiwa mara ya pili mfululizo.

Mnamo 2022-23, Vicario alifungwa mabao 39 kutokana na mechi 31 za Serie A. Hakufungwa goli katika mechi saba huku akisaidia Empoli kujivunia pengo la pointi 12 juu ya mduara uliojumuishwa vikosi vilivyoteremshwa ngazi.

Aliitwa katika kambi ya Italia kwa mara ya kwanza mnamo Septemba ambapo alipangwa katika kikosi cha akiba katika mchuano wa kufuzu kwa Euro ulioshuhudia Uingereza wakiwapokeza kichapo cha 1-0 nyumbani.

Tangu wakati huo, Vicario alipangwa katika kikosi cha akiba cha Italia kwenye michuano ya kirafiki dhidi ya Albania na Austria; na nusu-fainali ya UEFA Nations League mapema mwezi wa Juni 2023.

Fraser Forster, 35, ni kipa mwingine kambini mwa Spurs na ‘nyani’ huyo raia wa Uingereza aliwajibishwa pakubwa na Spurs mnamo 2022-23 baada ya Lloris kupata jeraha.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Wanawake wawili wafikishwa kortini kwa utapeli wa Sh15.6...

Polisi wanasa washukiwa 17 na misokoto 500 ya bangi katika...

T L