Na MASHIRIKA
ALAN Browne alitokea benchi na kufungia Jamhuri ya Ireland bao la pili katika sare ya 2-2 waliyoisajili dhidi ya Ubelgiji wanaoshikilia nafasi ya kwanza kimataifa kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).
Ubelgiji waliokuwa wakichezea ugenini walijiweka kifua mbele katika dakika ya 12 kupitia kwa Michy Batshuayi. Ingawa Chiedozie Ogbene alisawazishia Ireland katika dakika ya 35, Ubelgiji walijiweka uongozini kupitia kwa Hans Vanaken kunako dakika ya 58.
Mechi hiyo ilikuwa ya kwanza kwa Ireland kushiriki tangu Novemba 2021 safari yao ya kufuzu kwa fainali zijazo za Kombe la Dunia nchini Qatar mnamo Novemba-Disemba 2022 ilipokatika. Sare dhidi ya Ubelgiji iliendeleza rekodi ya kutoshindwa kwa Ireland kutokana na mechi saba zilizopita.
Ubelgiji walikosa huduma za wachezaji mahiri wakiwemo Kevin de Bruyne (Manchester City) na Romelu Lukaku (Chelsea) baada ya kocha Roberto Martinez kuunga kikosi kilichojumuisha wanasoka ambao hawakuwa wamechezea Ubelgiji zaidi ya mechi 50.
Jamhuri ya Ireland sasa wanajiandaa kuvaana na Lithuania kirafiki mnamo Machi 29, 2022 huku Ubelgiji wakipimana nguvu na Burkina Faso kabla ya kuelekeza makini kwa kipute cha UEFA Nations League mnamo Juni 2022.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO