• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Uhispania wakomoa Czech na kutua kileleni mwa Kundi A2 la Uefa Nations League

Uhispania wakomoa Czech na kutua kileleni mwa Kundi A2 la Uefa Nations League

Na MASHIRIKA

UHISPANIA walipepeta Jamhuri ya Czech 2-0 mnamo Jumapili usiku katika uwanja wa La Rosaleda jijini Malaga na kutua kileleni mwa Kundi A2 la Uefa Nations League.

Kiungo Carlos Soler wa Valencia alifungulia Uhispania ukurasa wa mabao kwa kujaza kimiani krosi ya Marco Asensio katika dakika ya 24 kabla ya Pablo Sarabia kutokea benchi na kufunga bao la pili la wenyeji.

Bao la Sarabia, 30, lilikuwa zao la ushirikiano mkubwa kati yake na fowadi matata wa Barcelona, Ferran Torres. Uhispania walianza mechi kwa matao ya juu na wakatamalaki mchuano huo kwa kumiliki asilimia mkubwa ya mpira.

Ingawa Jamhuri ya Czech walipata nafasi kadhaa za kufunga mwishoni mwa kipindi cha pili, walizipoteza fursa hizo kupitia Vaclav Cerny na Jan Kutcha.

Ushindi wa Uhispania wanaonolewa na kocha Luis Enrique uliwawezesha kuruka Ureno waliopokezwa kichapo cha 1-0 kutoka kwa Uswisi.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Ecuador kushiriki Kombe la Dunia 2022 baada ya FIFA...

MUME KIGONGO: Wataalamu sasa waonya kuwa kuumwa na kichwa...

T L