• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:55 AM
Vipusa wa Man-City na Chelsea kukutana kwenye nusu-fainali za Kombe la FA msimu huu

Vipusa wa Man-City na Chelsea kukutana kwenye nusu-fainali za Kombe la FA msimu huu

Na MASHIRIKA

MABINGWA watetezi wa Kombe la FA, Manchester City walifunga Leicester City mabao sita katika kipindi cha pili na kusajili ushindi wa 6-0 uliowakatia tiketi ya kuvaana na vipusa wa Chelsea kwenye nusu-fainali.

Baada ya kipindi cha kwanza kukamilika bila bao lolote, Khadija Shaw alifungua ukurasa wa magoli kabla ya mabao mengine ya kikosi hicho cha Gareth Taylor kufumwa wavuni kupitia Vicky Losada, Alex Greenwood, Filippa Angeldahl na Shaw aliyecheka na nyavu mara tatu.

Warembo wa Man-City walijitosa ugani kwa ajili ya mechi hiyo siku tatu baada ya kupepetwa 5-0 na Arsenal katika Ligi Kuu ya Uingereza (WSL).

Man-City wameshinda Kombe la FA mara mbili katika kipindi cha misimu miwili iliyopita na wameweka wazi azma ya kunyanyua taji hilo kwa mara ya tatu mfululizo licha ya kukutanishwa na Chelsea ambao pia wanajivunia ufufuo mkubwa wa makali yao.

Chini ya kocha Emma Hayes, Chelsea walifungiwa mabao na Sam Kerr pamoja na Fran Kirby na hivyo kusajili ushindi wa 4-0 dhidi ya Birmingham City mnamo Jumatano usiku na kufuzu kwa nusu-fainali dhidi ya Man-City.

Kerr na Kirby kwa pamoja wana jumla ya mabao tisa kufikia sasa msimu huu na wanategemewa pakubwa kuvunia Chelsea Kombe la FA kwa mara ya kwanza tangu 2016.

  • Tags

You can share this post!

Uholanzi kushirikiana na Kenya kuibuka na aina ya viazi...

Uhitaji wa jezi ya Ronaldo waongezeka kwa asilimia 3,000