• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Vipusa wafuzu tenisi ya Afrika

Vipusa wafuzu tenisi ya Afrika

NA GEOFFREY ANENE

TIMU ya taifa ya tenisi ya Kenya ilirejea nyumbani Jumatatu jioni kutoka nchini Rwanda ambako ilivuna medali ya dhahabu katika kitengo cha wasichana na fedha upande wa wavulana.

Katika makala hayo ya tano ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 12, Nancy Kawira, Natasha Akoth na Seline Ahoya walibwaga Burundi, Uganda, Tanzania na Rwanda kwa mechi tatu bila jibu kila mmoja.

Kenya ilikuwa inatetea taji hilo la wasichana.

Ushindi uliwezesha Kenya pamoja na nambari mbili upande wa wasichana Burundi kujikatia tiketi ya kushiriki mashindano ya Afrika mwezi Septemba katika nchi itakayotangazwa baadaye.

Uganda, Tanzania na Rwanda zilikamata nafasi tatu za mwisho upande wa wasichana mtawalia.

Kwa upande wa wavulana, Uganda ilinyakua taji ikifuatiwa na Kenya, Burundi, Rwanda na Tanzania mtawalia.

Kenya, ambayo iliwakilishwa hapa na Ainsley Elavuna, Ayaan Quadros na Jeff Okuku, haikuingia mashindano ya Afrika kwa sababu mshindi pekee katika kitengo cha wavulana ndiye aliyekuwa anafuzu kutokana na mashindano hayo ya Zoni ya Nne.

  • Tags

You can share this post!

Raila asisitiza Azimio itakuwa na mwaniaji mmoja kila kiti

TAHARIRI: Rais, Naibu wake wajue wanachojali wananchi ni...

T L