• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 5:55 AM
Wasichana wa Mukuru Talent wakata tikiti ya fainali

Wasichana wa Mukuru Talent wakata tikiti ya fainali

Na JOHN KIMWERE

KOCHA wa Mukuru Talent Academy, Amos Abong’o amesema kuwa wanataka kujituma mithili ya mchwa kupigania tikiti ya kufuzu kushiriki fainali za Ligi ya Daraja la Kwanza katika soka la wanawake.

Kipute hicho kimegawanywa katika makundi mawili A na B ambapo timu zitakaomaliza katika nafasi tatu za kwanza zitajikatia tikiti ya fainali. ”Wachezaji wangu nimewaambia kuwa lazima tupambane mwanzo mwisho endapo tunalenga kutimiza azma ya kufuzu kwa fainali,” jana alisema na kuongeza kampeni za msimu huu hakuna mteremko.

Alidokeza kuwa licha ya kupoteza mechi mbili mfululizo ana imani vigoli wake wakikaza buti watawapiku wapinzani na kumaliza kati ya tatu bora.Mukuru Talent ambayo imepangwa Kundi A imejikuta njiapanda ambapo mechi tatu za karibuni imevuna alama moja ilipotoka bao 1-1 na Msato Starlets.

Kisha kulala kwa mabao 4-1 na 2-1 mbele ya Soccer Sisters na Sunderland Samba mtawalia. Timu hiyo inashiriki kipute hicho kwa mara tatu mfululizo ambapo kwenye mechi za muhula huu inashikilia nafasi ya sita kwa kutia kapuni pointi tisa, moja mbele ya Limuru Starlets.

Nayo Msato Starlets inaburura mkia kwa alama sita baada ya kupiga patashika kumi. Kangemi Starlets ingali kileleni kwa alama 30 ambapo imeshinda mechi zote kumi ambazo imeshiriki. Sunderland Samba inafunga mbili bora kwa kuzoa pointi 22, tatu mbele ya MTG United.

  • Tags

You can share this post!

Matokeo mseto ya mechi mbalimbali yashuhudiwa ligini

Mwana habari na mwigizaji chipukizi anayepania kuzidisha...