• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 5:50 PM
West Ham kukutana na Viborg FF ya Denmark au B36 ya Faroe Islands katika mchujo wa Europa Conference League 2022-23

West Ham kukutana na Viborg FF ya Denmark au B36 ya Faroe Islands katika mchujo wa Europa Conference League 2022-23

Na MASHIRIKA

WEST Ham United watakutana ama na Viborg FF ya Denmark au B36 kutoka Faroe Islands katika raundi ya kwanza ya mchujo wa kufuzu kwa kipute cha Europa Conference League mnamo 2022-23.

Chini ya kocha David Moyes, West Ham walitinga nusu-fainali za Europa League mnamo 2021-22 ambapo walidenguliwa na miamba wa Ujerumani, Eintracht Frankfurt ambao hatimaye walitawazwa wafalme.

West Ham walikamilisha kampeni za EPL mnamo 2021-22 katika nafasi ya saba na kufuzu kwa kivumbi kipya cha Europa Conference League ambacho ni cha hadhi ndogo barani Ulaya baada ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) na Europa League.

Mechi za mchujo wa kufuzu kwa Europa Conference League 2022-23 zimeratibiwa kusakatwa kati ya Agosti 18-25, 2022.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Meneja wa New KPCU ataja mikakati yake ya kukabili wizi wa...

Maandalizi ya kura yashika kasi katika IEBC

T L