Na MASHIRIKA
WOLVERHAMPTON Wanderers wamemfuta kazi kocha Bruno Lage baada ya miezi sita pekee kutokana na msururu wa matokeo duni.
Kichapo cha 2-0 kutoka kwa West Ham United mnamo Jumamosi kilisaza Wolves katika mduara wa vikosi vitatu vya mwisho katika jedwali la Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) kwa alama sita, sawa na Crystal Palace waliopigwa na Chelsea 2-1 ugani Selhurst Park katika pambano jingine la EPL.
Kufikia sasa, Wolves wameshinda mechi moja pekee na kupoteza tisa kati ya 15 zilizopita ambazo wamesakata chini ya Lage aliyemrithi kocha Nuno Espirito Santo mnamo Juni 2021.
Wolves walioambulia nafasi ya 10 katika EPL mnamo 2022-23, wamefunga mabao matatu pekee kutokana na michuano minane iliyopita katika EPL muhula huu wa 2022-23.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO