NA WINNIE ATIENO
MWANIAJI wa Ugavana kaunti ya Mombasa, Bw Hezron Awiti amelalamika kuwa Gavana Hassan Joho anamzuia kumuona kinara wa chama cha ODM Bw Raila Odinga.
Alisema Bw Joho amekuwa akimwekea visiki asimfikie Bw Odinga.
“Haiwezekani kuwa unataka kura za jamii yetu ilhali hutaki tumfikie Bw Odinga,” alisema Bw Awiti.