• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 7:50 AM
Dkt Ruto amtembelea Rais anayeondoka Uhuru Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi

Dkt Ruto amtembelea Rais anayeondoka Uhuru Kenyatta katika Ikulu ya Nairobi

NA SAMMY WAWERU

RAIS atakayeapishwa kesho Jumanne Dkt William Ruto amemtembelea Rais anayeondoka Uhuru Kenyatta, katika Ikulu jijini Nairobi, Jumatatu.

Dkt Ruto amekaribishwa na kupokelewa na mwenyeji wake, Rais Kenyatta pamoja na mkewe, Margaret Kenyatta.

Ziara ya Ruto imejiri siku moja kabla ya kuapishwa rasmi, kuanza kuhudumu kama Rais wa tano wa Jamhuri ya Kenya.

Kesho, Jumanne, Septemba 13, 2022 atalishwa kiapo na Jaji Mkuu Martha Koome katika uwanja wa Kimataifa wa Moi, Kasarani jijini Nairobi.

Hafla hiyo ya kitaifa itatekelezwa kati ya saa nne asubuhi hadi saa nane mchana.

Wiki iliyopita, baada ya mahakama ya upeo kuidhinisha ushindi wa Ruto kufuatia kesi iliyowasilishwa na mpinzani wake, kinara wa Azimio la Umoja-One Kenya Alliance, Raila Odinga kupinga matokeo ya kura za urais, alisema “amekawia muda wa miezi kadhaa kabla kuzungumza na Rais kenyatta”.

Siku chache baadaye aliafikia ahadi yake kuzungumza na Rais anayeondoka, kwa njia ya simu.

Dkt Ruto alikuwa ameandamana na mkewe, Rachael Ruto na walitua Ikulu dakina chache baada ya saa kumi alasiri.

  • Tags

You can share this post!

Real Madrid yazamisha Mallorca na kuendeleza ubabe wao...

Rais Kenyatta ampongeza Dkt Ruto akimtakia kila la heri...

T L