• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 10:50 AM
Gachagua amsifu Rais Ruto akimtaja kama kiongozi atakayeimarisha Kenya 

Gachagua amsifu Rais Ruto akimtaja kama kiongozi atakayeimarisha Kenya 

NA SAMMY WAWERU

NAIBU wa Rais Rigathi Gachagua amemmiminia sifa Rais William Ruto, akimtaja kama kiongozi mchapakazi.

Akihutubu Jumanne katika uwanja wa Kasarani, Nairobi baada ya wawili hao kuapishwa, Bw Gachagua amesema Dkt Ruto ametekeleza vilivyo majukumu aliyopewa katika serikali za awali.

Bw Ruto amewahi kuhudumu kama Waziri wa Elimu na Kilimo, wakati wa utawala wa Rais mstaafu Mwai Kibaki ambaye kwa sasa ni marehemu.

Katika serikali ya Jubilee 2013 – 2022, iliyoongozwa na Rais ambaye ameondoka, Uhuru Kenyatta, alihudumu kama naibu wa rais.

“Ninaomba Wakenya msiniweke kwenye mizani mnilinganisha na rekodi ya utendakazi wa Rais William Ruto,” Gachagua akasema.

“Huenda nikazoa kati ya asilimia 60 – 70, na tunaposonga mbele ninahimiza Wakenya tufanye kazi kwa bidii,” akaelezea.

Naibu wa Rais vilevile amewataka Wakenya kupenda na kuthamini familia zao, akidai alipohangaishwa na serikali ya Jubilee mkewe na wanawe walisimama naye kidete.

“Mchunge familia zenu…Familia haiwezi ikakuacha unapopitia changamoto,” akasihi.

Bw Gachagua amekuwa akinyooshea kidole cha lawama serikali ya Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta, akisema imekuwa ikimhangaisha.

Katika awamu ya pili ya Jubilee, alihudumu Gachagua alikuwa Mbunge wa Mathira.

  • Tags

You can share this post!

Dkt Ruto aapishwa rasmi kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya...

Rais Ruto kuwateua haraka iwezekanavyo majaji sita...

T L