• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 1:01 PM
IEBC yakana ‘kumsaidia’ Ruto

IEBC yakana ‘kumsaidia’ Ruto

Na WANDERI KAMAU

TUME Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Jumanne ilikanusa madai kuwa inashirikiana kisiri na mrengo wa ‘Hustler Nation’ wake Naibu Rais William Ruto kumsaidia kuvumisha azma yake kuwania urais 2022.

Madai hayo yalienezwa kwenye mitandao ya kijamii, yakidai kuwa IEBC inausaidia mrengo huo kwenye harakati za kujiandaa kwenye uchaguzi huo.

Madai hayo, ambayo yalisambazwa kwenye mtandao wa Facebook, pia yalidai kuwa tume imefungua akaunti ya YouTube, kuusaidia kupeperusha masuala yanayohusiana na mipango yake.

Lakini kwenye taarifa, tume ilitaja madai hayo kuwa uvumi, ambapo lengo lake ni kuiharibia sifa.

“Madai yanayoenezwa dhidi yetu si ya kweli. Zaidi ya hayo, akaunti ya YouTube tunayodaiwa kuimiliki ni ghushi na si yetu. Tumeuarifu usimamizi wa YouTube kuhusu madai hayo ili kuwachukulia hatua wahusika,” ikaeleza tume.

Madai hayo yanajiri wiki chache baada ya wabunge kadhaa wa chama cha ODM kusema kuwa hawana imani na tume hiyo.

You can share this post!

Kipa Ederson Moraes sasa kudakia Man-City hadi 2026

Mudavadi kuteua mgombea mwenza kutoka Mlima Kenya