• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 10:55 AM
Kenya Kwanza wapiga abautani kuhusu mtaala

Kenya Kwanza wapiga abautani kuhusu mtaala

NA DERICK LUVEGA

VINARA wa muungano wa Kenya Kwanza wamebadili kauli kuhusu Mtaala wa Elimu ya Umilisi na Utendaji (CBC) huku wakisema hawataufutilia mbali iwapo watashinda urais katika Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9.

Kiongozi wa Amani National Congress (ANC) Musalia Mudavadi alisema Jumatano serikali ya Kenya Kwanza itaboresha mtaala huo.

Kulingana na Bw Mudavadi, mtaala wa CBC ambao umechukua mahala pa 8-4-4, ni ghali na unatatiza wazazi wengi wa mapato ya chini.

Awali, wanasiasa wa Kenya Kwanza walikuwa wameahidi kufutilia mbali kabisa mtaala wa CBC iwapo wataunda serikali ijayo.

Bw Mudavadi kupitia kwa msemaji wake Kibisu Kabatesi, alisema serikali yao itaufanyia marekebisho mtaala huo unaolenga kuwezesha vipaji vya watoto kutambuliwa mapema.

  • Tags

You can share this post!

Man-City waingia robo-fainali za UEFA licha ya Sporting...

Upungufu wa hela ulimsukuma Musalia kwa Ruto – Mbunge...

T L