• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 10:55 AM
MAANDAMANO: Raila ahutubia wafuasi Eastleigh, raia waliochoshwa na ugumu wa maisha wamshangilia

MAANDAMANO: Raila ahutubia wafuasi Eastleigh, raia waliochoshwa na ugumu wa maisha wamshangilia

NA MWANDISHI WETU

KIONGOZI wa Azimio La Umoja-One Kenya Raila Odinga ameingia jijini kwa kishindo huku waandamanaji wakimshangilia.

Msafara wake umeanzia katika hoteli ya Serena na amefululiza hadi katika mtaa wa Eastleigh.

Akihutubia wafuasi wa Azimio saa tisa, Raila amesema maandamano yatakuwa yakifanyika kila Jumatatu.

Amesema ni lazima serikali itimize ahadi zake na ishushe gharama ya maisha kwa Wakenya.

Amesema ni sharti masuala haya matano yashughulikiwe:

  1. Ruzuku ili bei za vyakula, bidhaa zishuke
  2. Serikali ipunguze ushuru
  3. Karo ipunguzwe elimu iwe nafuu
  4. ‘Server’ ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ifunguliwe
  5. Suala la uteuzi wa makamishna wa IEBC liangaziwe.
  • Tags

You can share this post!

Mandago adai nia ya Raila ni kuyumbisha serikali ya Ruto

Wafuasi wa Azimio Kilifi wataka Mnyazi, Chonga na Madzayo...

T L