• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 8:22 PM
Machifu: Naibu Rais ametutishia kwa simu

Machifu: Naibu Rais ametutishia kwa simu

STEPHEN MUNYIRI

HALI ya wasiwasi imewakumba baadhi ya maafisa wa utawala katika eneo la Mathira ambapo machifu wametishwa kutimuliwa kazi na Naibu Rais Rigathi Gachagua.

Kwa mujibu wa baadhi yao Bw Gachagua aliwapigia machifu simu aliodai walikuwa wanaunga mkono mrengo wa Azimio wakati wa kampeini za uchaguzi mkuu wa Agosti 9, 2022.

Machifu wawili – George Mukabi, Dadson Ithiru pamoja na naibu wa chifu Burton Chiuma – wamedai Bw Gachagua aliwapigia simu Jumatatu wiki hii na kuwaambia wakati wa “kulipiza kisasi ni sasa.”

Kulingana na ushahidi ulioshuhudiwa ni Taifa Leo, Bw Gachagua aliwapigia simu maafisa hao wa utawala kati ya saa mbili usiku na saa tatu unusu usiku.

Kisa cha kutishwa kwa machifu hao kilithibitishwa na Naibu Kamishna Mathira Mashariki Bw Peter Gicheha aliyesema walimweleza suala hilo lakini akasema hilo jambo la “kibinafsi kati ya Naibu Rais na maafisa hao wa utawala.”

  • Tags

You can share this post!

150 wameuawa katika hali tata, ripoti yasema

Heko japo kazi bado, mashirika ya kijamii yaambia magavana

T L