• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Mawaziri watatu wa Joho wajiuzulu kuwania viti

Mawaziri watatu wa Joho wajiuzulu kuwania viti

NA WACHIRA MWANGI

MAAFISA watatu katika Serikali ya Kaunti ya Mombasa, wamejiuzulu ili kuwania viti vya kisiasa.

Aliyekuwa Waziri wa Elimu katika kaunti hiyo, Dkt Seth Odongo, anataka ugavana wa Migori huku mwenzake wa Michezo, Jinsia na Vijana, Bw Innocent Mugabe, akimezea mate ubunge Likuyani, Kaunti ya Kakamega.

Kwa upande wake, Bw Patrick Mbelle aliyehudumia idara ya mawasiliano anataka kuwania udiwani katika eneo la Bamburi, Mombasa.

Bw Mugabe alitolewa kutoka Chuo Kikuu cha Kiufundi cha Mombasa ambapo alikuwa mhadhiri katika idara ya Utalii.

Amechangia pakubwa katika idara ya utalii ya kaunti hiyo ambapo alikuwa afisa mkuu kabla ya kuhamishwa hadi idara ya Michezo, Jinsia na Vijana.

“Nimejiuzulu ili kuingia katika siasa. Ajenda yangu kuu ni kuinua watu wa Likuyani na kulifanya eneo-bunge langu kuwa eneo bora la ICT na kilimo. Nitatumia tajriba yangu kuleta mabadiliko na maendeleo,” akasema Bw Mugabe.

Kwa upande wake, Bw Mbelle aliahidi kuleta mabadiliko. “Ninataka kupambana na viwango vya chini vya elimu na vilevile kutumia

ushawishi na mamlaka yangu katika bunge kusukuma utekelezaji wa ajenda ya uchumi wa baharini,” akasema Bw Mbelle.

  • Tags

You can share this post!

Alenga kutetemesha anga za uigizaji licha ya masaibu

Uhuru aanza kutoa Jubilee ICU

T L