• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
Mpinzani wa Mbadi ajiondoa na kumuunga mkono ugavana Homa Bay

Mpinzani wa Mbadi ajiondoa na kumuunga mkono ugavana Homa Bay

NA GEORGE ODIWUOR

KAMPENI za mwenyekiti wa ODM John Mbadi za kusaka ugavana wa Kaunti ya Homa Bay, zimepigwa jeki baada ya mshindani wake mmoja kujiondoa na kutangaza kumuunga mkono.

Mfanyabiashara Jared Kiasa, alijiondoa katika kinyang’anyiro hicho na kusema kuwa anampendekeza

Bw Mbadi kuiongoza kaunti kama gavana wa pili. Bw Kiasa alitoa tangazo hilo katika hafla moja mjini Homa Bay iliyohudhuriwa na Bw Mbadi, wanasiasa wengine na wafuasi wao.

Mbunge huyo wa Suba Kusini na Bw Kiasa ni miongoni mwa wawaniaji wanaotarajiwa kukabiliana katika mchujo wa kushindania tiketi ya ODM mnamo Agosti 18.

Wengine ni aliyekuwa Mbunge wa Kasipul Oyugi Magwanga, Mbunge Mwakilishi wa Kike wa Homa Bay Gladys Wanga, aliyekuwa Gavana wa Nairobi Evan Kidero, Katibu Mkuu wa chama cha kutetea masilahi ya walimu wa shule za upili (KUPPET) Akelo Misori na aliyekuwa Katibu wa kaunti ya Homa Bay Isaiah Ogwe. Wote hao wanapania kumrithi Gavana wa sasa Cyprian Awiti.

  • Tags

You can share this post!

Jubilee sasa mbioni kukabili UDA Bonde la Ufa

Mchujo UDA wazua hofu tele Pwani

T L