• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 5:17 PM
Mung’aro aahidi kuongeza bajeti ya sekta ya elimu akishinda Agosti

Mung’aro aahidi kuongeza bajeti ya sekta ya elimu akishinda Agosti

NA WINNIE ATIENO

MWANIAJI ugavana katika Kaunti ya Kilifi kupitia Chama cha ODM, Bw Gideon Mung’aro, ameahidi kuzingatia sekta ya elimu ili wanafunzi wote wanufaike na basari endapo atashinda uchaguzi wa Agosti.

Akiongea kwenye kampeni zake eneo la Rabai, Bw Mung’aro, alikosoa utawala uliopo unaoongozwa na Gavana Amason Kingi, akidai uliwekeza fedha kidogo kwenye bejeti ya elimu.

“Nitaongeza bajeti ya elimu hadi Sh20 milioni ili watoto wetu wote wanufaike na elimu ya bure. Wanafunzi wengi ni werevu sana lakini wanashindwa kukamilisha shule kwa sababu ya umaskini,” akasema.

  • Tags

You can share this post!

Naibu Gavana wa Mombasa adai kuhangaishwa na maafisa Kaunti

Ruto, Raila wahepa marafiki wa karibu

T L