• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 3:13 PM
Naibu Gavana wa Mombasa adai kuhangaishwa na maafisa Kaunti

Naibu Gavana wa Mombasa adai kuhangaishwa na maafisa Kaunti

NA FARHIYA HUSSEIN

NAIBU Gavana wa Mombasa, Dkt William Kingi, amedai kuhangaishwa na maafisa wa usalama wa kaunti hiyo.

Dkt Kingi ambaye ni mwaniaji ugavana Mombasa kupitia Chama cha Pamoja African Alliance (PAA), amedai kuwa maafisa walienda nyumbani kwake kuchukua gari lake rasmi la kazi bila kumwarifu.

“Ni haki yangu kuwa na magari hayo kwa sababu bado nawakilisha afisi ya Naibu Gavana wa Mombasa. Hakuna aliyeniarifu kuwa watachukua magari rasmi. Walikuja nyumbani kwangu wakati ambapo familia yangu ilikuwepo, hiyo haifai,” alisema Dkt Kingi.

Juhudi zetu kuthibitisha madai hayo kwa Serikali ya Kaunti ya Mombasa hazikufua dafu, kwani maafisa waliotafutwa hawakujibu simu.

Dkt Kingi alisema kuwa alilazimika kupeana gari moja kati ya mawili aliyokuwa amepewa na kaunti.

“Hii si mali ya mtu. Bado nahudumu katika afisi hiyo na nitawakabidhi nitakapomaliza muda wangu,” akasema.

Dkt Kingi amekuwa naibu wa Gavana Hassan Joho tangu uchaguzi wa 2017 ulipofanywa.

  • Tags

You can share this post!

Gavana Samboja kumenyana na wengine 12 Kaunti

Mung’aro aahidi kuongeza bajeti ya sekta ya elimu...

T L