• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Ruto arudi Taveta baada ya shamba lake kuibua gumzo

Ruto arudi Taveta baada ya shamba lake kuibua gumzo

LUCY MKANYIKA NA VALENTINE OBARA

NAIBU Rais William Ruto, Jumatatu alirudi tena Pwani kwa kampeni zake, siku chache tu baada ya msururu wa kampeni katika kaunti za ukanda huo wiki iliyopita.

Dkt Ruto na wandani wake wa muungano wa Kenya Kwanza walipigia debe azma yake ya urais katika Kaunti ya Taita Taveta.

Ziara hiyo ilitokea wakati ambapo hisia mseto bado zinatolewa baada ya naibu rais kufichua jinsi alivyopata shamba la takriban ekari 1,000 katika eneo hilo, aliyodai kupewa na aliyekuwa Mbunge wa Taveta, Bw Basil Criticos, alipomlipia deni katika Shirika la Kifedha la Kilimo (AFC).

Katika mikutano ya hadhara aliyofanya Jumatatu, Dkt Ruto anayewania urais kwa tikiti ya Chama cha United Democratic Alliance (UDA), alijipigia debe kwa msingi wa miradi iliyotekelezwa na serikali ya Jubilee, akisema amejitolea kuendeleza mbele miradi aina hiyo.

Alikuwa ameandamana na kinara wa ANC, Bw Musalia Mudavadi, Seneta wa Bungoma, Bw Moses Wetang’ula (Ford Kenya), Gavana wa Machakos, Dkt Alfred Mutua (Maendeleo Chap Chap), Gavana wa Kwale, Bw Salim Mvurya, miongoni mwa wengine.

  • Tags

You can share this post!

Jinsi unavyoweza kuhifadhi mboga na bidhaa za saladi kwenye...

Sina uadui na Ruto, asisitiza Mishra huku akiomba kura...

T L