NA WANDERI KAMAU
NAIBU Rais William Ruto na muungano wa Azimio la Umoja wameanza kuzozana kuhusu atakayeandaa mkutano wake wa mwisho wa kisiasa katika viwanja vya michezo vya Nyayo na Kasarani.
Hii ni baada ya Bodi ya Kusimamia Viwanja Kenya (SK) kusema viwanja hivyo vitakuwa vikitumika kwa “shughuli za kueneza amani nchini” kati ya Agosti 5 na 7.