NA WINNIE ATIENO
ALIYEKUWA gavana wa Nairobi, Bw Mike Sonko, amemtaka mgombeaji urais wa muungano wa Azimio la Umoja One Kenya, Bw Raila Odinga, kutoshinikiza kura za suti.
Kulingana naye, shinikizo hilo ni dhulma kwa wagombea wengine kwenye muungano huo wanaompigia debe kwa urais.
Huku akimfanyia kampeni Bw Odinga, aliwaomba pia wanasiasa waliotoroka Wiper na kuwa wagombeaji huru warudi katika chama hicho.
Mwanasiasa huyo angali anajitahidi kujumuishwa kwenye orodha ya wagombeaji ugavana Mombasa kupitia mahakama.