• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 6:09 PM
Tolgos atetea umaarufu wa Raila Rift Valley

Tolgos atetea umaarufu wa Raila Rift Valley

NA FRED KIBOR

MSHIRIKISHI wa Azimio la Umoja-One Kenya katika eneo la Bonde la Ufa, Gavana Alex Tolgos, amepuuzilia mbali dhana kwamba eneo hilo ni ngome ya chama cha United Democratic Alliance (UDA) na Naibu Rais William Ruto.

Bw Tolgos ambaye ni gavana wa Elgeyo Marakwet, alisema kinyume na chaguzi zilizopita, Bw Odinga atapata kura nyingi zaidi katika eneo hilo lenye jumla ya kura 5.9 milioni.

“Katika chaguzi zilizopita eneo hilo limekuwa likipiga kura kwa misingi ya msisimko wa vyama. Hali hiyo imebadilika sasa. Wapiga kura sasa wanalenga kuwachagua watu binafsi jinsi itakavyodhihirika katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9,” Bw Tolgos akaambia Taifa Leo jana Jumatano.

“Tumetangamana na wapiga kura katika kampeni zetu na kubaini kuwa misimamo yao imegeuka. Hamu yao ni kuchagua viongozi ambao wataweka mbele masilahi yao.“Wanahisi kudanganywa na ndio maana wanashabikia urais wa Raila,” akasema.

Bw Tolgos alisema yeye na wenzake wameweka mikakati itakayomwezesha Bw Odinga kupata zaidi ya asilimia 40 ya kura zote katika eneo hilo.

  • Tags

You can share this post!

Urais: Midahalo ya wawaniaji wenza wa mirengo tofauti...

Sterling kirasmi aingia Chelsea

T L