NA JAMES MURIMI
RAIS William Ruto ametangaza kwamba chama cha United Democratic Alliance (UDA) kitafanya uchaguzi wake wa kitaifa mnamo Desemba 2023.
Amefichua hayo Jumamosi baada ya kufungua ofisi kubwa ya chama hicho katika eneo la King’ong’o, Kaunti ya Nyeri.
“Uchaguzi huo utaimarisha demokrasia ndani ya chama cha UDA tunapojiandaa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2027,” amesema Rais Ruto.
Kiongozi wa nchi amewataka wagombea wa nyadhifa mbalimbali na wanachama wa UDA kujiandaa kikamilifu.
Chama cha UDA kiko ndani ya muungano tawala wa Kenya Kwanza ambao viongozi wake waliunda serikali baada ya kubwaga Azimio La Umoja-One Kenya unaoongozwa na Raila Odinga wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM).