Na WACHIRA MWANGI
VIONGOZI wa kidini kutoka Kaunti ya Mombasa wametoa wito kwa Rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake Dkt Willam Ruto waridhiane kwa ajili ya umoja wa taifa hili.
Wakiongozwa na Askofu wa Kanisa la KNCPCM Dkt Stanley Michuki, walisema kuwa uhasama wa kisiasa kati ya viongozi hao wawili unatishia umoja wa nchi na huenda ukaishia kwenye ghasia.
“Kama viongozi wa dini ambao huombea nchi hii, tunakerwa na uhasama kati ya Rais Kenyatta na Dkt Ruto,” akasema Askofu Dkt Michuki.