• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 9:17 PM
Wagombeaji ugavana Homa Bay wakimbilia koo kujitafutia uungwaji 2022

Wagombeaji ugavana Homa Bay wakimbilia koo kujitafutia uungwaji 2022

Na GEORGE ODIWUOR

KINYANG’ANYIRO cha ugavana wa Homa Bay kimeshika kasi huku wagombeaji wakisaka uungwaji mkono kutoka kwa koo na familia kuelekea uchaguzi mkuu wa 2022.

Mwanasiasa wa hivi punde kuidhinishwa na watu wa ukoo ni Mbunge Mwakilishi wa kaunti hiyo Gladys Wanga ambaye ni mmoja wa wagombeaji wenye ushawishi mkubwa.

Wagombeaji wengine ambao wamepata uungwaji kutoka kwa wanachama wa koo mbalimbali ni Katibu wa Kaunti ya Homa Bay Isaiah Ogwe na mfanyabiashara Jared Kiasa ambao wameidhinishwa na wazee wa koo za Kanyada na Kanyamwa, mtawalia.

Hatua ya Bi Wanga kuidhinishwa na ukoo wa Kochia ni ya kipekee ikizingatiwa kuwa asili yake ni kaunti ya Kisumu.

Mbunge huyo Mwakilishi alizaliwa katika kijiji cha Wang’aya, eneobunge la Muhoroni na ameolewa katika eneobunge la Rangwe, kaunti ya Homa Bay, ambako wanaishi watu wa ukoo wa Kochia.

Wanawake wamekuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi wanapowania viti nje ya maeneo ambako walizaliwa.

Walioathirika zaidi ni wale wanaomezea mate viti vya ugavana katika eneo zima la Luo Nyanza, hali inachangia wengi kudinda kuwania kiti hicho.

Hata hivyo, wazee wa ukoo wa Kochia walisema wanapambana na taasubi za kiume kupitia hatua yao ya kumwidhinisha Bi Wanga kwa kiti cha ugavana wa Homa Bay.

Wazee hao ambao pia ni wanachama wa Baraza la Wazee la Waluo walimwishinisha Bi Wanga katika sherehe iliyohudhuriwa na wakazi wengi wa Homa Bay.

You can share this post!

Kimunya apuuza waundao vyama vidogo Mlimani

Magavana wa Pwani wapata presha kali kuungana

T L