• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
Wanga kuapishwa wafanyakazi wa kaunti wakigoma

Wanga kuapishwa wafanyakazi wa kaunti wakigoma

NA GEORGE ODIWUOR

GAVANA mteule wa kaunti ya Homa Bay Gladys Wanga wiki hii ataanza majukumu yake bila huduma kutolewa kwa wakazi.

Hii inafuatia mipango ya wafanyakazi wa serikali ya kaunti kugoma kwa kutolipwa mishahara yao. Bi Wanga ataapishwa Alhamisi kuanza rasmi majukumu ya gavana.

Hata hivyo kuapishwa kwake kunajiri wakati ambao wafanyakazi wa idara tofauti za kaunti wamegoma na wakazi kukosa kupata huduma. Gavana anayeondoka Cyprian Awiti ataachia serikali mpya madeni. Miongoni mwa madeni hayo ni kukosa kulipa wafanyakazi ambao wametishia kulemaza huduma wakati ambao serikali mpya itaanza kazi. Wafanyakazi katika kaunti hiyo wanataka serikali kuwalipa mishahara ya Julai na Agosti.

Kupitia chama cha Watumishi wa Umma, wafanyakazi hao wamelalamikia hatua ya serikali inayoondoka ya kutowalipa mishahara kwa wakati jambo ambalo wanasema linaathiri maisha yao ya kila siku.

Katibu wa tawi la Homa Bay la chama hicho Tom Aketch alisema kwamba wafanyakazi wa kaunti wanakumbwa na matatizo ya kiuchumi kwa sababu ya kutolipwa mishahara yao.

  • Tags

You can share this post!

Wapigakura Mlima Kenya walivyotimua madiwani wengi

Ngoma yaanza

T L