NA BRIAN OJAMAA
BARAZA la Wazee wa jamii ya Waluhya limemfokea Naibu Rais William Ruto kwa kumshambulia Rais Uhuru Kenyatta katika mikutano ya kisiasa.
Wazee hao, wakiongozwa na mwenyekiti wao, Bw Patrick Wangamati, walimwonya Ruto dhidi ya ‘kumkosea heshima’ Rais.
Wazee hao waliokuwa wakizungumza kijijini Khachonge, Kaunti ya Bungoma, walidai kuwa matamshi ya hasira ambayo yamekuwa yakitolewa na Dkt Ruto ni tishio kwa amani na utulivu wa nchi.