• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Uingereza yawapa onyo raia wake kuhusu shambulio la kigaidi Kenya

Uingereza yawapa onyo raia wake kuhusu shambulio la kigaidi Kenya

Na STELLA CHERONO

UINGEREZA imetoa tahadhari ya usafiri kwa raia wake wanaoishi ama wanaotembelea Kenya dhidi ya tishio la ugaidi na utekajinyara.

Aidha, taifa hilo liliwashauri kuwa waangalifu dhidi ya mashambulio ya kundi la kigaidi la Al Shabaab, kwani huenda wakalenga baadhi ya maeneo muhimu kama hoteli, vilabu, maduka ya jumla, na maeneo ya Pwani kama fuo za bahari.

“Mashambulio hayo huenda yakawa katika maeneo ya kuabudu; kama vile makanisa na misikiti, kwani yamekuwa yakilengwa. Mnapaswa kuwa na tahadhari kubwa,” ikasema taarifa.

Tahadhari hiyo inajiri baada ya Inspekta Jenerali wa Polisi Joseph Boinnet kutangaza kwamba vikosi vya usalama vimefanikiwa kuzima shambulio kubwa la kigaidi ambalo lilipangiwa kutekelezwa jijini Nairobi.

Kufikia sasa, zaidi ya watu 12 wamekamatwa kwa kuhusishwa na shambulio hilo ambapo wamefikishwa mahakamani lilifanyika baada gari moja lililojaa vilipuzi kunaswa katika eneo Merti, Isiolo.

 

You can share this post!

Wazee wateta kunyimwa hela kwa sababu ya vidole chakavu

Wanasiasa wataka Jubilee iwe macho Raila asije akazima...

adminleo