• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:50 AM
GOLD COAST AUSTRALIA: Ni shaba tu kwa bondia Christine

GOLD COAST AUSTRALIA: Ni shaba tu kwa bondia Christine

Na CHRIS ADUNGO

BONDIA Christine Ongare aliwaepushia wanamasumbwi wa Kenya aibu ya kuambulia pakavu kabisa katika ulingo wa ndondi baada ya kumdengua Jumatano Dulani Jayasinghe wa Sri-Lanka katika ukumbi wa Oxenford Studios.

Ongare ambaye kwa sasa ana uhakika wa kutia kapuni angalau nishani ya shaba, anataingia katika nusu-fainali ya pili mnamo Ijumaa adhuhuri dhidi ya Carly McNaul wa Ireland Kaskazini.

Licha ya kukabiliwa na presha ya kufanya vyema katika fani hiyo baada ya wawakilishi wengine 10 wa Kenya kubanduliwa mapema, Ongare alimzidi maarifa Jayasinghe kwenye robo-fainali ya kitengo cha uzani wa kilo 51.

Refa  Valeri Pastuhov kutoka Jamhuri ya Moldova alilazimika kusitisha mapema mchuano huo baada ya Ongare kumwelekezea Jayasinghe makonde yaliyomlemea mapema.

Elizabeth Andiego wa Kenya na mwenzake Lorna Simbi walibanduliwa na Millicent Agboegbulem (Nigeria) Marie-Jeanne Parent wa Canada mtawalia.

You can share this post!

GOLD COAST AUSTRALIA: Unyonge wa Wakenya mbio za masafa...

Chiloba sasa amshtaki Chebukati

adminleo