• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Wabunge walalamikia kuachwa kwa mabwanyenye ndani ya Mau walalahoi wakifurushwa

Wabunge walalamikia kuachwa kwa mabwanyenye ndani ya Mau walalahoi wakifurushwa

Na Anita Chepkoech

WABUNGE wawili wa Jubilee wamelaumu serikali kwa kufurusha maskini kutoka Msitu wa Mau na kuwaacha mabwanyenye.

Mbunge wa Konoin Brighton Yegon na mwenzake Maalum Gideon Keter walisema mabwanyenye 25 walio na ushawishi serikalini wametengewa jumla ya hekta 500 ndani ya Msitu wa Mau na hawajaathiriwa na operesheni inayoendelea ya kuwafurusha wakaazi.

Wanasiasa hao walidai kuwa miongoni mwa mabwanyenye hao ambao wanaendelea kuendesha shughuli zao ni Seneta, aliyekuwa msaidizi wa rais na mbunge; ambao hawakuwataja.

Viongozi hao walikuwa wakizungumza katika eneo la Mogogosiek, Konoin wakati wa uzinduzi wa tovuti ya eneobunge itakayotumika kuweka rekodi ya miradi inayoendeshwa na Hazina ya Ustawishaji wa Maeneobunge (NG-CDF).

“Operesheni ya kuhamisha watu kutoka Msitu wa Mau inaonekana kuwa na njama fiche ya kisiasa. Wamiliki wa mashamba makubwa ndani ya msitu hawajaguswa ilhali wamiliki wa mashamba madogo ambao ni maskini wanafurushwa,” akasema Bw Yegon.

Takribani watu 10,000 wamefurushwa kutoka Msitu wa Mau katika juhudi za kutaka kuokoa ekari 46,000 ambazo ni chanzo cha maji.

Bw Keter alisema kuwa kubatilishwa kwa baadhi ya hatimiliki za mashamba ni ishara kwamba serikali iliwahadaa hivyo maskini hawapaswi kuadhibiwa kutokana na uozo katika wizara ya Ardhi.

You can share this post!

Atwoli akana kutoroka na mke wa watu

Mudavadi adai Raila aliwaficha kuhusu muafaka

adminleo