• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 8:50 AM
Jicho Pevu aahidi maskwota ardhi akisema Ruto atainunua ili wagawiwe

Jicho Pevu aahidi maskwota ardhi akisema Ruto atainunua ili wagawiwe

NA WINNIE ATIENO

MBUNGE wa Nyali, Bw Mohammed Ali ameapa kusaidia maskwota kutoka kijiji cha Soweto, Kadzandani ambao wanalumbana na mmiliki wa ardhi.

Bw Ali alitoa mfano wa zaidi ya ekari 1, 000 za Kwa Bulo ambazo zilikuwa na utata akisema umetatuliwa baada ya Rais William Ruto kuingilia kati na suluhu ikapatikana.

“Hapa Soweto, kama mwenyewe ana hati miliki, nitamtafuta tufanye mazungumzo ili tuelewane. Baadaye nitaenda kufanya mazungumzo na Rais anunue hii ardhi kwa mwenyewe alafu ikabidhiwe kwa wakazi,” alisema Bw Ali.

Hata hivyo, Bw Ali alisema endapo mwenye ardhi hiyo hana hatimiliki, wakazi hawataondolewa kwenye ardhi hiyo yenye utata.

 

  • Tags

You can share this post!

Masoja waomba kumiliki bastola badala ya nyongeza ya...

Nduguye mbunge wa Kilome ni miongoni mwa walioangamizwa na...

T L