• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Uhuru na Ruto wajiuzulu ikiwa hawawezi kushirikiana – Karua

Uhuru na Ruto wajiuzulu ikiwa hawawezi kushirikiana – Karua

Na Wanderi Kamau

KIONGOZI wa Narc-Kenya, Bi Martha Karua, amesema Rais Uhuru Kenyatta ameonyesha mfano mbaya katika uzingatiaji wa Katiba kwa kumtenga Naibu Rais William Ruto katika uendeshaji wa serikali.

Kwenye mahojiano jana, Bi Karua alisema Rais Kenyatta amevunja sheria kwa kumtenga Dkt Ruto. Bi Karua alisema kuwa ijapokuwa wawili hao wameruhusiwa kutofautiana kuhusu masuala fulani, wanapaswa kubuni ushirikiano katika utendakazi wao kwa manufaa ya Wakenya.

Alisema ikiwa watafeli kufanya hivyo, basi wanapaswa kujiuzulu na kuwapa nafasi wananchi kuwachagua viongozi watakaofanya kazi kwa ushirikiano mzuri.

“Ikiwa watashindwa kushirikiana, basi wajiuzulu na kuwapa Wakenya nafasi kuwachagua viongozi wapya. Walichaguliwa pamoja, hivyo wanapaswa kufanya kazi kwa ushirikiano. Ikiwa rais anahisi hawezi kushirikiana na naibu wake, na ikiwa (rais) anahisi naibu amefanya kitendo kinachokiuka Katiba, basi anapaswa kubuni mchakato wa kumwondoa mamlakani au ashirikiane naye,” akasema.

Uhusiano wa wawili hao ulianza kudorora Machi 2018, baada ya Rais Kenyatta kubuni handisheki na kiongozi wa ODM, Raila Odinga.

 

You can share this post!

Afueni kwa wavuvi kiwanda kikikamilika

Wakereketwa wa BBI waomba kukubaliwa kucheza reggae