• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Fiji wahifadhi nishani ya dhahabu kwenye raga ya Olimpiki

Fiji wahifadhi nishani ya dhahabu kwenye raga ya Olimpiki

Na MASHIRIKA

FIJI walipokeza New Zealand kichapo cha 27-12 na kutwaa dhahabu ya pili ya Olimpiki katika historia ya taifa hilo.

Fiji ilijishindia dhahabu ya kwanza kwenye Olimpiki miaka mitano iliyopita baada ya raga kujumuishwa kwenye michezo ya Olimpiki kwa mara ya kwanza. Fiji inajivunia idadi ya watu wasiozidi milioni moja pamoja huku ikikabiliwa pia na changamoto za uchache wa rasilimali.

Semi Radradra wa klabu ya Bristol ni miongoni mwa wanaraga wa Fiji wanaodumishwa kwa mshahara wa juu zaidi katika ulingo wa raga.

Chini ya kocha Gareth Baber ambaye ni raia wa Wales, Fiji watakosa makaribisho sawa na yale ambayo kikosi kilichozoa dhahabu ya Olimpiki miaka mitano iliyopita nchini Brazil kilipokezwa.

Kufikia Machi 2021, Fiji haikuwa imetikiswa hata kidogo na janga la corona huku vifo viwili pekee vikiripotiwa. Hata hivyo, idadi ya vifo iliongezeka na kufikia 200 tangu wakati huo huku kukiwa na hofu kwamba huenda sekta ya afya ikalemewa.

Uingereza waliokuwa wakipigiwa upatu wa kuzoa dhahabu waliambulia pakavu baada ya kupigwa 17-12 na Argentina katika mchuano wa kuwania nishani ya shaba.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Kenya Lionesses wazidiwa maarifa na New Zealand raga ya...

Ni wale wale wa ahadi hewa 2022