NA DENNIS SINYO
MASABA, CHEPTAIS
JOMBI aliyekuwa na mazoea ya kubeba vidosho bila kuwalipisha kwenye pikipiki yake, ameacha kazi hiyo baada ya petroli kupanda bei.
Kulingana na mdokezi, jamaa alikuwa na mazoea ya kubeba akina dada bila malipo.
Wenzake walimuonya tabia hiyo ingemletea hasara lakini aliwapuuza.
Majuzi, jamaa aliamua kuacha biashara hiyo kwa kukosa pesa za kununua petroli.
Aliambiwa, “Umejistaafisha mapema kwa kuweka tamaa mbele.”