• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 5:46 PM
Kalameni akemea ex wake kwa kumwandama warudiane

Kalameni akemea ex wake kwa kumwandama warudiane

MTWAPA MJINI

Na JANET KAVUNGA

KALAMENI wa hapa alimfokea demu aliyemtema kwa kumwandama akitaka kujua vipusa anaotoka nao.

Mwanadada alivunja uhusiano wake na jamaa mwaka jana lakini amekuwa akichunguza mienendo yake chini ya maji hadi kalameni akagundua na kumkabili.

“Koma kuweka makachero kunifuatafuata. Uhusiano wangu na wewe uliisha uliponiacha kwa madharau na sasa niko na uhuru wa kufanya nitakacho na kutoka na nimtakaye,” jamaa alimweleza demu ambaye alishtuka ishara kwamba hakutarajia Kalameni kuwa mkali kwake.

Juhudi za demu kumtaka jamaa atulie wazungumze wazike tofauti zao ziligonga mwamba na marafiki zake wakamwambia alikosea kwa kumtema jamaa.

***

Msupa akataa kupatanishwa na jombi mtoro

KHAYEGA, KAKAMEGA

Na TOBBIE WEKESA

KIKAO cha patanisho kilichoandaliwa eneo hili kiligeuka uwanja wa fujo kipusa alipotofautiana na wazee. Inadaiwa kipusa aliamrisha wazee wa ukoo kuondoka mara moja kabla hajawachukulia hatua.

Duru zinasema wazee waliandaa kikao cha kumpatanisha kipusa na bwanake baada ya wawili hao kuwa na mzozo uliosababisha polo kugura boma.

“Sisi tuko hapa kuwapatanisha. Hatufurahii bwanako akiishi mbali na wewe. Anafaa kurudi kwa boma,” wazee walieleza.

Habari zinasema kipusa aliinuka na kudai kwamba amezoea kuishi peke yake na hahitaji mume tena.

“Kama hilo ndilo lililowaleta hapa siwataki. Nani aliwaambia namhitaji! Ondokeni haraka,” kipusa alifoka.
Inadaiwa kikao kilitamatishwa ghafla na kila mtu akaenda zake.

  • Tags

You can share this post!

Garissa, Kwale zilikuwa na watahiniwa wengi walio na umri...

Viongozi Uasin Gishu wasukuma Serikali iongeze bei ya...

T L