• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 5:50 AM
Kwayamasta nusura aharibu ndoa yake ‘mpango’ alipoamua kumwanika baada ya kumtema

Kwayamasta nusura aharibu ndoa yake ‘mpango’ alipoamua kumwanika baada ya kumtema

Na JANET KAVUNGA

MOMBASA MJINI

UHUSIANO wa pembe za chaki wa mwanadada na kiongozi wa kwaya ya kanisa lao ulifichuka jamaa alipomtema demu huyo naye akamwanika hadharani.

Wanakwaya wengine walishangaa kugundua kwamba mwenzao alikuwa akichepuka na kwayamasta kwa miaka kadhaa hadi pale jamaa alipomtema na kuamua kuzingatia familia yake.

“Iliibuka kwamba jamaa alikuwa akimtunza demu kwa kila kitu lakini alipoondoa ufadhili wake, mwanadada alikasirika kwa kukosa maisha ya hali ya juu aliyokuwa akifurahia. Aliamua kumuaibisha jamaa bila kujua kwamba alikuwa pia akijifedhehesha kwa kutoka na mume wa mtu,” alisema mdokezi.

Inasemekana mzee wa kanisa aliingilia kati kutuliza demu kabla ya mke wa jamaa kupata umbea.

  • Tags

You can share this post!

Rais Ruto aelekea nchini China kupalilia uhusiano na...

Serikali kukwamua vyuo vikuu kwa ufadhili wa Sh90 bilioni

T L