NA JANET KAVUNGA
SHANZU, MOMBASA
MWANADADA wa hapa alijuta kumtema mumewe baada ya kuhadaiwa na mpango wake wa kando kuwa angeacha mkewe waoane.
Demu huyo alianza uhusiano na jamaa wakati ambao alikuwa ametofautiana na mumewe.
Jamaa alimwambia hata yeye alikuwa amekosana na mkewe na angemtaliki. Alimshawishi mwanadada kumtema mumewe ili waoane akimtaliki mkewe.
Demu alidhani alikuwa ameangukia bahati kwa kuwa jamaa alikuwa na mshahara mnono kuliko mumewe na alikuwa akimnunulia zawadi na kumfadhili starehe za kila aina.
Hata hivyo, baada ya kumtema mumewe, jamaa alianza kumuonyesha dharau huku akimfisia mkewe kila wakati akiwa na demu huyo.
Demu alipomtaka atimize ahadi yake, jamaa alim-block kabisa ikawa vigumu kumpata kwenye simu na mitandao ya kijamii.
Alijaribu kurudi kwa mumewe ambaye alikataa kwa sababu alikuwa amegundua uhusiano wake na jamaa huyo. Kwa sasa demu amebaki kwa mataa.