• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 1:01 PM
DONDOO: Ndoa yadumu wiki 2 tu demu akidai jembe la mume ni butu

DONDOO: Ndoa yadumu wiki 2 tu demu akidai jembe la mume ni butu

EMBU MJINI

NA LEAH MAKENA

KIDOSHO wa hapa alishangaza kuendea pasta wake akitaka amsaidie kupata talaka, wiki mbili tu baada ya kufunga ndoa.

Inasemekana kidosho huyo alinyooshea pasta kidole cha lawama akisema ndiye alimshauri wasifanye “majaribio” kuona jinsi ngoma inadunda kabla ya harusi yao.

“Huu mzigo wa kushughulikia talaka tutaubeba mimi na wewe kwa pamoja sababu ni wewe ulinipotosha,” demu aliteta.

“Ningeonjesha hilo dume asali mapema ningejua jembe lake halilimi vizuri,” akasema.

Duru zinaeleza kuwa licha ya mwanadada kufanyiwa ushauri nasaha ili avumilie mumewe kwa muda atunze ndoa yake, alidinda kabisa akisema hakuwa tayari kuishi na dude lisilomtosheleza.

***

Vipusa wahepa mwenzao aliyewekwa kinyumba na mwanamume aliye na mke

SOTIK MJINI

NA NICHOLAS CHERUIYOT

KIPUSA amejipata mpweke baada ya mashoga wake kumhepa alipowekwa kimada na jombi aliye na mke.

Duru zasema urafiki wa kidosho na wenzake ulitumbukia nyongo walipogundua amekubali kuwekwa kinyumba na mwanamume wa mtu.

“Kidosho alitongozwa na jombi na akameza chambo mara moja bila kujali alikuwa na mke. Hatukufurahia kabisa uamuzi huo na tukaamua kumuambaa,” alieleza rafiki mmoja wa demu.

Demu alipokataa ushauri wao walimtenga na kumuonya acheze mbali nao kwani walitaka kudumisha maadili yao.

***

Polo azua rabsha mazishini sababu ya kukosa minofu

KAPTICH, NAKURU

NA NICHOLAS CHERUIYOT

POLO wa hapa alinguruma katika hafla ya mazishi alipoagizwa afuate laini ya kupata mlo wa wali na maharagwe, baada ya kuzuiwa kuingia ndani ya nyumba kuu ili ale minofu na wadosi.

Jamaa huyo aliteta vikali kwamba alitoa pesa nyingi katika mchango wa kufanikisha mazishi hayo, ilhali sasa anasukumwa nje asile vitamutamu.

“Siku ya harambee mlishangilia nilipotoa elfu tano lakini sasa hamnitambui!” aliwaka polo asijali wageni waliokuwepo katika hafla hiyo ya maombolezo.

“Eti mapochopocho ni ya wadosi! Hao wadosi walitoa nini siku ya harambee?” akaongeza huku ametoa sura kali kuelekea familia ya mwendazake.

Hatimaye, jombi aliruhusiwa kujumuika na wadosi ndani ya nyumba wakashambulia nyama na sembe.

***

Ushindwe! Msupa azima kaka mtoro aliyejifanya mlokole amuingize boksi

BAMBURI, MOMBASA

NA JANET KAVUNGA

DEMU alinyamazisha kalameni mkora aliyejifanya ameokoka ili apate fursa ya kumrushia chambo.

Mwanadada huyo alimfokea kalameni huyo baada ya kugundua kwamba yeye hufika kanisani tu ili aonekana Mkristo imara bali lengo ni amuingize boksi.

Inasemekana jamaa alikuwa amemrushia chambo mwanadada huyo ambaye tunafahamishwa ameokoka kindakindaki.

Aidha, mabarobaro wengi wameogopa kumtupia mistari kidosho kwa sababu anashikilia kwa dhati imani yake.

Kalameni akajipiga kifua kwamba yeye atapenya; akaanza kwenda kanisani lengo likiwa kumnasa demu, lakinin akala hu!

“Najua unajifanya tu umeokoka ila unanitaka. Ushindwe kabisa! Yule alikuambia ukija kanisani nitakupenda alikudanganya. Jaribu kwingine,” demu alimzima polo.

 

  • Tags

You can share this post!

Wanaume hawawezi kustahimili habari mbaya kama wanawake...

Ruto atoa ahadi mpya kwa Wapwani huku wakazi wakimtajia...

T L