• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 6:55 AM
Pasta ageuka mgonganishaji wa waliopoteza mpendwa wao

Pasta ageuka mgonganishaji wa waliopoteza mpendwa wao

NA CORNELIUS MUTISYA

IVETI, MACHAKOS

PASTA mmoja eneo hili, aliwaudhi waombolezaji alipodai marehemu alitolewa kafara na jamaa wake.

Pasta aliponyanyuka kuhubiri alishangaza waombolezaji kwa kutapika nyongo.

“Jamaa huyu ametolewa kafara na jamaa wake ili azidi kuwa tajiri. Tunakemea nguvu za giza ambazo zimetamalaki eneo hili,’’ pasta alihubiri.

Penyenye za mtaa zaarifu kuwa, waombolezaji walisinywa na mahubiri hayo na wakaanza kumzomea pasta kwa kupanda mbegu ya chuki katika familia ya marehemu.

‘‘Haufai kamwe kugonganisha wanafamilia kwa kudai marehemu alitolewa kafara. Huu ni uchochezi wa hali ya juu,’’ mzee mmoja alimwambia pasta huku waombolezaji wakishangilia lakini mazishi yakaendelea ilivyokuwa imepangwa.

  • Tags

You can share this post!

Fanyeni kazi au muende nyumbani, gavana wa Isiolo aonya

Waislamu wakerwa na hatua ya mahakama kuwapa mashoga uhuru...

T L