• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 3:55 PM
Chipukizi wa  AFC Leopards Youth wazidi kutamba Ligini

Chipukizi wa AFC Leopards Youth wazidi kutamba Ligini

Na JOHN KIMWERE

VIJANA wa AFC Leopards Youth wamejiongezea matumaini ya kujikatia tiketi ya fainali za kipute cha Nairobi West Regional League (NWRL) baada ya kuliza Kibera Golden mabao 3-1 ugani Ligi Ndogo, Nairobi.

Timu hiyo ya kocha, Martin Aganda anazidi kukaza buti inakolenga kubeba tiketi ya kufuzu kupandishwa ngazi kushiriki Ligi ya Taifa Daraja la Pili muhula ujao. Nayo Makarios 111 FC (Riruta United) ilipata pigo kwa kudondosha alama tatu muhimu baada ya kuzabwa mabao 2-1 na 360 Media FC uwanjani Ruiru Stadium mjini humo.

Kwenye patashika ya AFC, chipukizi hao wanaoshikilia uongozi wa ngarambe hiyo walitembeza soka safi na kutia kapuni pointi tatu kupitia Maxwell Otieno aliyepiga kombora mbili huku Victor Otieno akifunga bao moja.

”Ninashukuru wachezaji wangu kwa kazi nzuri wanaoendelea kufanya kwenye kampeni za msimu huu,” kocha wa AFC alisema na kuongeza kuwa hawana la ziada ila wamepania kupambana mwanzo mwisho kuhakikisha wamenasa tiketi ya kusonga mbele.

Kadhalika anatoa wito kwa wachezaji wake kushiriki mechi zote kama fainali maana vikosi vyote vinazidi kujituma kwa udi na uvumba. Alikiri wazi kuwa kampeni za msimu huu zimeshuhudia ushindani mkali kinyume na ilivyokuwa muhula uliyopita.

Picha/JOHN KIMWERE
KAPETI: Kocha wa Redcarpet, Meshack Osero Onchonga na wachezaji wake.

Kwenye mfululizo wa matokeo hayo, Silver Bullet ilipigwa mabao 2-1 na Amazon Tigers, Maafande wa Nairobi Prisons walivuna ushindi sawa na huo mbele ya Re Union FC, Gachie Soccer iliendelea kudorora pia kuburura mkia ilipokubali kulala kwa mabao 3-1 mikononi mwa Uthiru Vision FC.

  • Tags

You can share this post!

Penye nia pana njia

Wanavoliboli wa Kenya ya ufukweni hawana corona, watawania...