• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 11:13 AM
DCI yachunguza kisa cha watoto kufungwa

DCI yachunguza kisa cha watoto kufungwa

Na STEVE NJUGUNA

IDARA ya Upelelezi Nchini (DCI) imeanzisha uchunguzi kuhusu kisa ambapo walimu wawili waliwafunga wanafunzi watatu wa Shule ya Msingi ya Thiru, Laikipia Magharibi, mitini kama adhabu ya kuchelewa kufika shuleni.

DCI jana ilianzisha uchunguzi dhidi ya Mwalimu Mkuu Shelmith Thimba na Naibu wake David Maina ambao wanadaiwa kuwafunga wanafunzi hao Ijumaa wiki jana.

Picha zilizosambaa mitandaoni zilionyesha wanafunzi hao watatu wakiwa wamefungwa kwa kamba mtini na kuzua ghadhabu miongoni mwa Wakenya.

Inadaiwa kuwa Naibu Mwalimu Mkuu alichukua picha za wanafunzi hao wa kisha akazituma kwenye ukumbi wa WhatsApp za wanafunzi hao kabla mwalimu mmoja kuzisambaza mitandaoni.

Hapo jana, maafisa wa DCI pamoja na Naibu Kamishina wa Kaunti ya Laikipia Moses Muroki walifika shuleni humo inayopatikana kilomita 15 kutoka mji wa Nyahururu.

Waliwahoji walimu pamoja na wanafunzi kuhusu kisa hicho hicho kilichokashifiwa na Wakenya na kutajwa kama tukio la uhayawani.

“Tumebaini kuwa ni kweli wanafunzi hao walifungwa mtini Ijumaa . Ni jambo la kukera na hatulifurahi hata kidogo. Tunasikitika kuwa wanafunzi hao walipitia hali kama hiyo. DCI imeanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo,” akasema Bw Muroki.

Mkurugenzi wa Shirika la Watoto Kaunti ya Laikipia Ezekiel Mwanza na mkurugenzi wa Tume ya Kuwaajiri Walimu (TSC) Irene Kadenge walikashifu kufungwa kwa wanafunzi hao wakisema ni jambo lisilothamini ubinadamu.

“Inashangaza kuwa watoto wetu wanapitia katika hali hiyo shuleni. Kama shirika la watoto tunakemea kitendo hicho na lazima tuwalinde watoto wetu,” akasema Bw Mwanza.

Alisisitiza kuwa shirika hilo litawalinda watoto hao watatu kisha kuwapa ushauri na nasaha na kufuatilia masomo yao .

You can share this post!

Mwanawe waziri wa zamani aponyoka kitanzi

Ukitapeliwa pesa kwa simu ni heri uzisahau tu – DCI