• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 2:21 PM
Gachagua aingia Harambee House Annex kwa kicheko na tabasamu

Gachagua aingia Harambee House Annex kwa kicheko na tabasamu

NA SAMMY WAWERU

NAIBU Rais Rigathi Gachagua atakuwa akiendelezea majukumu yake katika afisi rasmi za Harambee House Annex, badala ya mtaa wa kifahari wa Karen, jijini Nairobi.

Bw Gachagua ametoa tangazo hilo Jumatatu, akithibitisha kuhamia Harambee Annex.

Rais William Samoei Ruto, akihudumu kama Naibu Rais kwa kipindi kirefu kuanzia mwaka 2013 alikuwa akifanyia kazi katika Harambee House Annex japo alihamishia shughuli zake nyingi katika afisi ya Karen iliyokuwa imetengewa Naibu Rais. Hili kwa kiasi kikubwa lilitokea wakati uhusiano wake na Rais wakati huo – Uhuru Kenyatta – kuonekana kutofautiana naye kwa maswala mengi.

“Nitakuwa nafanyia kazi kwa ofisi yangu mpya Harambee House Annex, majukumu yameanza,” Gachagua akachapisha kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii, akishukuru wahudumu wa afisi ya naibu rais kumhakikishia kushirikiana naye kufanyia Wakenya kazi.

“Ninashukuru maaskofu kwa kuitakasa afisi yetu mpya, na kuikabidhi kazi yetu kwa Mwenyezi Mungu ninaposaidia Rais William Ruto kuhudumia taifa hili tukufu,” linaelezea chapisho la Naibu wa Rais.

Duru zinaarifu kiongozi wa Amani National Congress (ANC) Musalia Mudavadi ambaye huenda atateuliwa Mkuu wa Mawaziri wakati Dkt Ruto atabuni baraza la mawaziri, atakabidhiwa afisi hizo zilizoko Karen.

  • Tags

You can share this post!

Gachagua adai hana chuki binafsi na Uhuru

TALANTA: Gwiji wa zumari

T L