NA HILLARY KIMUYU
MKURUGENZI wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji amesema atatoa uamuzi iwapo idara hiyo itamshtaki aliyekuwa Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang’i kuhusiana na uvamizi unaodaiwa kufanyika nyumbani kwake katika mtaa wa Karen.
Hii ni baada ya mawakili wa Dkt Matiang’i kusema polisi walikuwa wamesema watamshtaki kwa makosa mawili.