• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 7:50 PM
Huzuni mkazi wa Witeithie akiuawa na fisi

Huzuni mkazi wa Witeithie akiuawa na fisi

Na LAWRENCE ONGARO

WAKAZI wa kijiji cha Witeithie wameachwa na mshangao baada ya mkazi mmoja wa eneo hilo kuliwa na fisi mnamo Jumapili usiku.

Kulingana na wakazi wa eneo hilo, mwanamume huyo alikuwa ameandamana na mwenzake ambaye alihepa mauti na akatoka kwenye mkasa.

Ilidaiwa kuwa wawili hao walikuwa wakirejea nyumbani majira ya usiku eneo la Kamuthi na ghafla wakapatana na fisi wapatao 20 waliokuwa wakizurura kichakani.

Katika hali hiyo, mwanamume mmoja alivamiwa na fisi hao ambao walimrarua na kumla.

Jamaa huyo mwingine alitoroka ambapo alieleza wanakijiji kuhusu mkasa huo.

Wakazi hao walipokwenda mahali pa tukio walikuta marehemu tayari ameliwa na fisi hao.

Mwili huo wa marehemu ulipelekwa kwa chumba cha kuhifadhi maiti cha General Kago mjini Thika.

Tayari afisi ya Idara ya Upelelezi mjini Juja imeanza uchunguzi ili kubaini jinsi tukio hilo lilitendeka.

Hata hivyo, maafisa wa idara ya polisi, na wale wa Shirika la Huduma kwa Wanyamapori (KWS) wameanza uchunguzi maalum ili kubaini chanzo cha tukio hilo.

Wakazi wa Witeithie wameshauriwa wawe watulivu ili uchunguzi wa kina ufanywe.

Wakazi wengi wa eneo hilo wameachwa na hofu.

  • Tags

You can share this post!

Visa 103 vya maambukizi mapya ya virusi vya corona...

Raila na Ruto bega kwa bega

T L