Na GEORGE MUNENE
WAKAZI walijawa na huzuni kutokana na kisa ambapo naibu chifu aliuawa kwa kudungwa kisu kufuatia mzozo wa kinyumbani katika kijiji cha Githure, kaunti ya Kirinyaga.
Ilidaiwa kuwa afisa huyo wa utawala, Denis Magu, 36, alishambuliwa kwa kisu na mkewe Jumatano usiku.
Alifariki alipofikishwa katika kituo cha afya cha Nuclear Medical Clinic.
Kulingana na mashahidi, Bw Magu aligombana na mkewe kuhusiana na mambo ya kinyumbani, mwendo wa saa tatu za usiku.
Walipigana baada ya kugombana na kuchangia kifo cha naibu huyo wa chifu wa kata ndogo ya Nyangeni katika eneo bunge la Gichugu.
Majerani walielezea jinsi mkewe alitwaa kisu cha jikoni wakati wa mapigano hayo na kumdunga mumewe kifuani.