• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 7:55 PM
Kijana wa miaka 15 afariki baada ya kugusa waya wa umeme

Kijana wa miaka 15 afariki baada ya kugusa waya wa umeme

NA MERCY KOSKEI

MVULANA mwenye umri wa miaka kumi na tano ameaga dunia baada ya kugusa waya wa umeme katika kijiji cha Wi-Rakuom, eneobunge la Ndhiwa, Kaunti ya Homa Bay.

Castro Odhiambo, mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi ya Wi-Rakuom alifariki baada ya kushika waya uliokuwa umetelekezwa kwenye makazi ya jirani yao.

Kulingana na naibu wa chifu wa eneo hilo Bw Alphonse, Odhiambo alikuwa amefika kwa jirani huyo kucheza na marafiki zake kabla ya kushika waya huo kwa kutumia ufimbo wa mbao.

Alisema kuwa marehemu alipiga mayowe baada ya kunaswa na umeme, hali iliyofanya marafiki zake na familia kukimbilia eneo la tukio.

Walimkuta amelala chini akiwa amepoteza fahamu.

Alikimbizwa katika hospitali ya kibinafsi ya Rodi Kopany ambapo madaktari walitangaza kuwa alifariki alipofikishwa kabla hata hajahudumiwa.

Mwili wa marehemu ulipelekwa katika hifadhi ya maiti ya Manyatta Kobodo.

 

  • Tags

You can share this post!

Rais Ruto na naibu wake Gachagua watoa Sh5 milioni kusaidia...

Kipkemboi, Jebet wapepea Nairobi City Marathon 2023, Tanui...

T L