• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 6:00 PM
Korti yaelezwa jinsi mwanamke alivyoibia mfanyabiashara

Korti yaelezwa jinsi mwanamke alivyoibia mfanyabiashara

Na JOSEPH NDUNDA

MFANYABIASHARA raia wa Uganda aliibiwa Sh130,000 na mwanamke saa chache baada ya kukutana kwa mara ya kwanza katika baa moja eneo la Kilimani, Nairobi.

Mwanamke huyo, Clare Monyangi Moseti, 28, anakabiliwa na shtaka la wizi katika Mahakama ya Kibera baada ya kudaiwa kwamba alimlewesha mfanyabiashara huyo katika nyumba yake iliyoko barabara ya Muringa, Kilimani, Nairobi.

Inadaiwa kwamba alitenda kosa hilo kati ya Oktoba 14 na 16 mwaka huu wa 2021.

Mfanyabiashara huyo yuko Nairobi kwa shughuli za kikazi na alikuwa akinywa pombe katika kilabu kimoja kilichoko Adlife Plaza wanawake wawili walipojiunga naye.

Aliketi nao wakilewa na akaomba mmoja nambari ya simu.

Alienda naye katika nyumba yake walipoendelea kuburudika hadi siku iliyofuata mwanamke huyo alipomwambia hakuwa ametosheka na pombe na wakaenda katika baa nyingine.

You can share this post!

WASONGA: Sherehe bila kusaidia familia za mashujaa ni kazi...

Agizo la Joho kuhusu miraa lapingwa vikali

T L