• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 7:15 PM
Makahaba waliopora mwanamume Sh250, 000 Makutano ya Mwea wakamatwa

Makahaba waliopora mwanamume Sh250, 000 Makutano ya Mwea wakamatwa

NA MWANGI MUIRURI
KAHABA wawili wanaodaiwa kupora mwanamume Sh250, 000 wlaitiwa nguvuni wikendi eneo la Makutano, katika mpaka wa Kaunti za Kirinyaga na Embu.

Kukamatwa kwa wawili hao kulitandaza hali ya taharuki miongoni mwa makahaba wa mji huo ambao baadhi yao wana kashfa za uporaji wakionekana kusafiri kuhepa msako huo.

Wanawake hao wawili walidaiwa kuwa kutekeleza wizi huo mnamo Juni 30, 2023 kupitia simu ya mkono ya mlalamishi.

Kwa mujibu wa Naibu Kamishna wa Kaunti Ndogo ya Mwea Bi Jane Manene, wanawake hao waliripotiwa kunyemelea namba za siri za kutoa pesa kutoka kwa rununu ya jamaa huyo.

“Habari tulizo nazo ni kwamba wawili hao wakishirikiana pamoja walihamisha pesa hizo kutoka kwa akaunti ya simu ya mwanamume huyo na kisha wakazigawana,” akasema.

Aliongeza kuwa walitoroka mji huo lakini baada ya muda wakarejea na ndipo wapelelezi wakawakamata.

“Uchunguzi sasa umezinduliwa rasmi kujua hali halisi ambayo pesa za mwanamume huyo zilihamia kwa simu ya mmoja wa washukiwa na ambaye alituma nusu yake kwa mshukiwa wa pili,” akasema.

Visa vya wanaume kuporwa pesa taslimu na pia kutoka kwa akaunti za benki na simu zimekuwa za kawaida katika mji huo.

Aidha, wanaume walio na pesa kufungiwa katika madanguro ya ukahaba wakiporwa ni baadhi ya changamoto za wateja wa mahaba eneo la Makutano

 

  • Tags

You can share this post!

Maelfu ya kampuni zafungwa kufuatia hali ngumu

Jaji asukumia Koome kesi ya Sheria ya Fedha 2023

T L