• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 8:55 PM
Mgomo wa wahadhiri wasitishwa kupisha mashauriano ya mishahara

Mgomo wa wahadhiri wasitishwa kupisha mashauriano ya mishahara

Na Francis Mureithi

MUUNGANO wa Wahadhiri wa Vyuo Vikuu nchini (UASU) jana ulisitisha kuwa mgomo uliotarajiwa kuanza leo huku pakiwapo hofu ungelemaza shughuli za mafunzo na masomo katika vyuo vikuu vyote 35 vya umma.

Kupitia taarifa, Katibu wa Kitaifa wa Uasu Dkt Constatine Wasonga alisema muungano huo ulifikia hatua hiyo ili kupisha mashauriano zaidi kati yake na wawakilishi wa serikali.

‘Kamati Kuu ya UASU imeamrisha kuwa muungano usitishe mgomo ili kuruhusu mazingumzo zaidi,’ akasema Dkt Wasonga.

Maafisa wakuu wa Uasu mnamo Jumapili jioni waliandaa mkutano na Katibu katika Wizara ya Elimu anayesimamia Elimu ya Juu na Utafiti, Simon Nabukwesi.Lengo la mkutano huo lilikuwa kutathmini hatua zilizochukuliwa na Wizara ya Leba kuanza utekelezaji wa mkataba wa nyongeza ya mshahara (CBA) ambao uliafikiwa hapo awali.

Kutotekelezwa kwa makubaliano hayo na usimamizi wa vyuo vikuu 35 ndiko kulikochochea Uasu kutoa notisi ya mgomo mnamo Agosti 23, ikidai wanachama wake wanaumia kimapato.

 

You can share this post!

Kagwe atishia kuadhibu walipishao chanjo

Hichilema aanza kazi kwa kishindo, atimua polisi na...